Ethiopia:tumaini linaongezeka katika makubaliano ya amani huko tigray - | vatican news

Vaticannews

Ethiopia:tumaini linaongezeka katika makubaliano ya amani huko tigray - | vatican news"

Play all audios:

Loading...

Pamoja na matumaini kuanza kuongezeka katika makubaliano ya amani huko Tigray, Ethiopia,lakini watu wamechoka sana na mzozo na wakati huo huo kuhitaji msaada wa kibinadamu.Kuna vita vingi


ambavyo havizungumzwi na vyombo vya habari na mitandao ya kijamii,ukiongeza umaskini na hali ngumu kutokana na vita nchini Ukraine na Urussi. NA ANGELLA RWEZAULA;– VATICAN. Pamoja na


matatizo makubwa yanayosababishwa na mgogoro, mabadiliko ya tabianchi, ukame mkali unaoathiri nchi idadi ya watu inapata ahueni angalau kwa ukweli kwamba inaanza kupumua hewa ya amani.


Wamekaribisha maendeleo ya mikataba ya amani kwa ujasiri. Na sasa wanasubiri kwa matumaini kwamba matokeo yanaweza kuonekana. Watu wamechoshwa na vita, ambavyo vimeharibu maisha, mali,


uhusiano kati ya jamii. Hivyo ndivyo anavyoripoti Padre Teshome Fikre Woldetensae, Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu wa Ethiopia, ambaye alikutana na waandishi wa habari wa Shirika la Habari


za Kimisionari wakati wa Mkutano wa Caritas Internationalis uliohitimishwa hivi karibuni jijini Roma ambao uliongozwa na mada “Kwa pamoja tutumikie kwa upendo”. Msafara wa Magari kutoka


Kamati ya Msalaba mwekundu kuanza kusambaza msaada huko Makelle,Tigray. Kanisa la Ethiopia linahusika hasa katika kutatua migogoro ya Tigray na katika eneo la Oromia magharibi mwa nchi,  


alisema Katibu, akikumbuka hali nyingi za dharura zinazoonesha hali ya sasa ya kihistoria kwamba kutokana na vita imeongezeka. idadi ya watu waliohamishwa. Baadhi yao bado wako mashambani,


wengine wanarudi makwao. Kwa sasa tunakabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa, huku ukame ambao umekuwa mkali sana. Jambo hilo linaathiri zaidi maeneo ya kusini na mashariki mwa nchi. Pia


wanakabiliwa na athari kubwa kutokana na mgogoro wa vita kati ya Urussi na Ukraine, ambayo imesababisha kuongezeka kwa gharama ya maisha duniani kote, na kusababisha umaskini zaidi. Msafara


wa Magari kutoka Kamati ya Msalaba mwekundu kuanza kusambaza msaada huko Makelle,Tigray. Kuhusu hali ya shule na elimu, Padre Teshome Fikre Woldetensae alisisitiza tatizo la shule ambazo


zimefungwa kwa miaka mingi katika maeneo mengi nchini, kutokana na UVIKO-19 na migogoro wao.  Kwa maana hiyo alisema kwamba katika miaka ya hivi karibuni wamejaribu kusaidia watoto na


wakimbizi wa ndani katika kambi ambao wananyimwa kila kitu, hata bidhaa za msingi. Zaidi ya hayo, kutokana na ukame, familia nyingi zimepoteza rasilimali zao, mifugo yao, na matokeo yake


kuongezeka kwa viwango vya utapiamlo kwa watoto na wazee. Kanisa linajaribu, pamoja na Caritas ya parokia, kulisha watoto wengi iwezekanavyo, katika familia, shuleni na katika kambi za


wakimbizi. Kuhusu maafikiano hayo ya amani, Padre huyo alionesha maneno ya kitulizo. Katika miaka miwili iliyopita wamesikia kuhusu vita tu, uharibifu, usaliti, na sasa, hata kusikia kwamba


vikundi viwili vinavyopigana vinakutana kujadili amani tayari ni tumaini. Wanaendelea kutumaini na kuomba kwamba hili lifanyike. Wanatumai kuwa mifumo itaundwa ili kuthibitisha utimilifu


mzuri wa ahadi na ahadi zilizotolewa na wahusika. Matokeo chanya ya kwanza yanakuja, mikonodo ya kibinadamu iko wazi na mashirika mengi yanatuma msaada wao kupitia misafa ya wa walinzi.


Kanisa Katoliki pia linachangia, kwa ushirikiano wa karibu na washirika wa kimataifa waliopo nchini. Kwa sasa kuna na dhamira ya kisiasa, na nia ya vyama ambavyo vimekuwa na migogoro, ambapo


si kuweka maslahi yao wenyewe katikati bali ya wananchi, maskini na wale wanaoteseka, kila kitu kinaweza kuanza kujitatua kwa urahisi zaidi. Watu wao wana furaha, kwa sababu wao ndio


wamelipa bei chungu zaidi. Maskini, ambao wamepoteza mali zao zote, ambao wamekufa katika vita na ugomvi.” Msafara wa Magari kutoka Kamati ya Msalaba mwekundu kuanza kusambaza msaada huko


Makelle,Tigray. Akiendelea kueleza laisema inawezekana kuwa na kushuka kwa kasi kama ilivyo katika mazungumzo yote, alisisitiza Padre Fikre,  lakini anaona kuwa kuna maslahi na dhamira ya


kisiasa kwa pande zote mbili, na jumuiya ya kimataifa imefanya kazi kwa njia ya kutia moyo ili pande zinazozozana ziingie kwenye mazungumzo na kuingilia kati njia ifaayo ya kushughulikia


dharura za kibinadamu. Tigray inakabiliwa na wakati wa matumaini makubwa, pia kutokana na usaidizi unaowasili. Katibu wa Baraza la Maaskofu Ethiopia aòobainisha kuwa  Kanisa daima limekuwa


upande wa watu, na Askofu wa Upatriaki wa Adigrat yupo, na wamisionari wapo pale! Kulingana na uwezekano wanadumisha mawasiliano kulingana. Wanawasiliana na wahudumu wa majimbi  na mashirika


 wanapopata fursa. Tumejaribu njia zote zinazowezekana ili kupata misaada ya kibinadamu. Walipowatuma wamisionari na washiriki wao huko Tigray, ilitokea kwamba walikutana na Patriaki


Tesfaselassie Medhin. Julai iliyopita mkurugenzi wa Caritas Ethiopia alikuwa Adigrat, pamoja na mameneja wa Caritas nyingine, na walizungumza naye, ambaye kwa hakika ana matatizo mengi. Kila


kitu kinakosekana huko, na yeye, kama mchungaji ambaye ni miongoni mwa watu wanaoteseka, sasa hana uwezekano wa kufanya chochote na anajuta. Lakini Kanisa lipo. Maaskofu wote wa Ethiopia na


Baraza la Maaskofu, kupitia Caritas, wamejaribu kufanya kila linalowezekana kutoa usaidizi na kushiriki mateso yao. Padre Fikre ameongeza kuwa, kwa bahati mbaya, maumivu na kukata tamaa


haviko katika Tigray pekee kwani bado kuna vita vingine vinavyoendelea katika eneo la magharibi mwa nchi, ambavyo hakuna vyombo vya habari vinavyozungumzia na hakuna shirika la kimataifa


linalovutiwa nalo. Kuna watu wengi waliokimbia makazi yao, na wengi wanakufa kila siku katika mapigano ya msituni katika eneo hilo. Kwa kuwa sasa mzozo wa Tigray umekuwa na mwonekano wa


kimataifa, lazima pia waaangalie mifuko mingine ya migogoro ambayo sehemu nyingine nyingi za nchi zinahusika. Kwa ujumla, umakini mdogo umelipwa kwa dharura hiyo, bado kuna msaada mdogo wa


kibinadamu kwa watu waliohamishwa. Tena, hiyo ni hali mbaya sana ambapo waathirika ni wakulima maskini. Vita na msaada mkoa wa Tigray Ethiopia Kaskazini


Trending News

Papa:wayahudi na wakristo wanaokiri muumba mmoja wanaweza kufungua njia za amani! - | vatican news

Katika mkutano na wawakilishi wa Jukwaa la Kimataifa la Kiyahudi,Papa Francisko amebainisha kwamba kila vita siku zote,k...

404 - ukurasa haujapatikana

Nenda kwenye maudhuiNenda kwenye orodha kuuNenda tovuti zaidi za DWVidio zetuSauti zetuMaeneoTanzaniaKenyaJamhuri ya Kid...

Papa Francisko:Teknolojia zijali kwanza kiini cha mwanadamu

2024.02.12 Papa alikutana na wajumbe washiriki wa Mkutano Mkuu wa Baraza la Chuo cha Kipapa cha Maisha,   (Vatican Media...

Uchaguzi Mkuu Tanzania 2020 – DW

Nenda kwenye maudhuiNenda kwenye orodha kuuNenda tovuti zaidi za DWVidio zetuSauti zetuMaeneoTanzaniaKenyaJamhuri ya Kid...

Congo Drc:hakimu ambaye alikuwa akichunguza kifo cha Attanasio ameuawa !

Damu zaidi katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Drc bado inamwagika. William Assani, hakimu wa jeshi ambaye a...

Latests News

Ethiopia:tumaini linaongezeka katika makubaliano ya amani huko tigray - | vatican news

Pamoja na matumaini kuanza kuongezeka katika makubaliano ya amani huko Tigray, Ethiopia,lakini watu wamechoka sana na mz...

Idhaa ya Kiswahili 12.07.2020 - | Vatican News

Podcast Idhaa ya Kiswahili 12.07.2020 Your browser does not support the audio element Mchango wako kwa ajili ya utume mp...

Linda Hassani | Premiere.fr

Biographie News Photos Vidéos Films Séries Nom de naissance Hassani Avis PoorNot so pooraveragegoodvery good Vidéo à la ...

Urusi yashambulia kituo cha kuhifadhi gesi ukraine

Hayo yamejiri wakati maafisa wakirejesha huduma za umeme katika miji, kuamuru ununuzi wa umeme na kuweka utaratibu wa mg...

Katekesi ya baba mtakatifu francisko tarehe 11 desemba 2019 - | vatican news

__ The portal Vatican News uses technical or similar cookies to make navigation easier and guarantee the use of the serv...

Top